|
SCUULT watoa kiasi cha shilingi milioni 700
2008-05-06 15:26:43
Na ITV Habari
Shirikisho la vyama vya akiba na mikopo SCUULT limefanikiwa kutoa kiasi cha shilingi milioni mia saba ikiwa ni utekelezaji wa programu ya utoaji wa mikopo kwa mikoa mbalimbali inayopatiwa fedha za uwezeshaji zilizotengwa na serikali kwa ajili ya kukopesha wajasiriamali.
Hayo yameelezwa na afisa masoko wa SCUULT Bw. Florian Haule wakati akitoa tathmini ya utoaji wa fedha hizo za uwezeshaji ambazo SCUULT ni miongoni mwa asasi zilizochaguliwa katika kusaidia ukopeshaji wa mabilioni ya fedha za uwezeshaji wananchi yanayotolewa na serikali.
|