|
Tumieni fursa ya EU wajasiriamali wasindikaji-Naiko
2008-05-06 15:25:56
Na ITV Habari
Watanzania wametakiwa kutumia fursa inayotolewa na jumuiya ya Ulaya ya kutafuta wajasiriamali wasindikaji katika sekta ya kilimo ili kufanya nao biashara katika sekta mbalimbali hapa nchini na Afrika kwa ujumla kupitia mkutano mkubwa wa wastani wa wafanya biashara 500 kutoka nchi za Afrika na Ulaya utakaofanyika hapa nchini kuingia ubia katika usindikaji mazao ya kilimo.
Mkurugenzi wa kituo cha uwekezaji nchini-TIC Emanuel Ole Naiko amesema hayo wakati akitoa hotuba ya ukaribisho kwa ujumbe wa wafanyabiashara kutoka jumuiya ya Ulaya na Wafanyabiashara na makampuni kutoka Afrika ambao wanakutana kubadilishana uzoefu na kufanya biashara na makampuni ya Afrika.
|