|
Asilimia 98 ya dawa hazithibitishwi ubora wake kabla ya kuingia sokoni
2008-03-19 11:13:56
Na ITV Habari
Asilimia 98 ya dawa zinazotakiwa kuthibitishwa ubora wake kabla ya kuingia sokoni zimebainika kuwa na kemikali hatari za sumu zinazochangia kusababisha madhara makubwa kiafya.
Hayo yamebainishwa jijini Dar es Salaam na katibu mkuu wizara ya afya na ustawi wa jamii, Bw. Wilson Mukama wakati akizundua kamati maalum ya kitafa ya kusimamia kemikali na kuwataka kutotoa vibali vya dawa hizo kuingia sokoni.
Wakitoa ufafanuzi wa utendaji kazi wa kamati hiyo itakayokuwa chini ya mkemia mkuu wa serikali, wakala wa usalama wa afya kazini Dk. Peter Riwa amesema kuna idadi kubwa ya kemikali za viwandani zinazozagaa katika maeneo ya makazi ya watu ambazo hazijahifadhi vizuri na hivyo kuhatarisha za afya za watu.
|