|
Hubert Kairuki inaendelea na zoezi la kupima kansa ya shingo ya uzazi
2008-02-08 12:21:38
Na ITV Habari
Taasisi ya afya na tiba ya Hubert Kairuki ya Mikocheni jijini Dar es Salaam imeendesha zoezi la kupima kansa ya shingo ya uzazi kwa kina na bila malipo kama sehemu ya maadhimisho ya kumbukumbu ya miaka tisa ya kifo cha muasisi wa hospitali hiyo Prof. Hurbert Kairuki.
Akizungumza katika zoezi hilo mjane wa marehemu na mwenyekiti wa bodi ya taasi hiyo Bibi Kokushubira Kairuki, amesema taasisi pia inafanya maonyesho mbalimbali ya masomo ya tiba.
|