|
Taifa Stars kukutana na timu kutoka Malawi
2008-02-02 11:39:30
By ITV Habari
Timu ya soka ya taifa ya Malawi inatarajiwa kuwasili nchini kesho kwa ajili ya mchezo wa kujipima nguvu dhidi ya timu ya taifa ya Tanzania- Taifa Stars, mechi itakayopigwa kwenye uwanja wa taifa jijini Dar es Salaam.
Afisa habari wa shirikisho la soka Tanzania- TFF, Florian Kaijage amesema hayo jijini Dar es Salaam alipokuwa akizungumzia ujio wa timu hiyo.
Aidha ametangaza kuongezwa kwa wachezaji wawili Godfrey Boniface na Juma Jabu katika kikosi cha Taifa Stars.
|