|
Rais Kikwete ametaka mazungumzo kati ya vyama vya CUF na CCM kupatakana muafaka
2008-05-16 15:34:15
Na EAR Habari
Rais Jakaya Kikwete wa Tanzania ametaka mazungumzo kati ya vyama vya CUF na CCM ili kupatakana muafaka kuendelea na majadiliano hayo ambayo anaamini kuwa yatazaa matunda mazuri kwa mustakabari wa Tanzania.
Katika taarifa iliyotolewa na Ikulu,inasema rais alitoa kauli hiyo alipokuwa na majadiliano na waziri wa nchi wa Ufaransa anayeshughulikia nchi zinazozungumza kifaransa, kuwa tofauti iliyojitokeza ni namna ya utekelezaji wa muafaka huo.
Rais Kikwete amesema kuwa uamuzi wa kuwa na serikali shirikishi Zanzibar ulichukuliwa miaka saba iliyopita, wakati wa majadiliano yaliyozaa muafaka wa kwanza kati ya CCM na CUF.
|