|
Mazungumzo ya amani baina ya serikali ya Uganda na waasi yameingia siku ya tatu
2006-07-16 18:59:50
Na EAR Habari
Mazungumzo ya amani baina ya serikali ya Uganda na waasi wa Lords Resistance Army LRA, leo yameingia siku ya tatu ya majadiliano ya kina, baada ya kufunguliwa rasmi ijumaa iliyopita.
Katika mazungumzo hayo ujumbe wa serikali ya Uganda unaongozwa na Waziri wa Mambo ya Ndani Dakta Ruhakana Rugunda, wakati waasi hao wanaongozwa na Bw. Martin Ojul.
Mazungumzo hayo yanafuatiliwa na makundi mengi, ambapo iwapo yatafanikiwa, yatafanikisha kumaliza vurugu na mateso yaliyodumu kwa miaka 20, kwa wananchi waishio kaskazini mwa Uganda.
|