08 May 2008 MAIN PAGE SITE INDEX CONTACT US HELP
  Swahilinews
NAVIGATION
SEARCH
 
SPECIAL  
ARCHIVES  
Print this article Send this article

Dodoma yapeta
 
2008-05-08 14:42:36
Na Azizi Issa

Mkoa wa Dodoma umevuna lengo la uzalishaji kwa asilimia 100 baada ya kubuna tani milioni 1.2 za mazao ya chakula.

Mkuu wa mkoa huo, William Lukuvi, amesema kuwa kiwango hicho ni kile kilichozalishwa mwaka jana.

Aidha, akasema mwishoni mwa mwaka huu kutakuwa na upungufu mkubwa wa chakula nchini.

Akawataka wananchi mkoani humo kutumia kwa uangalifu chakula watakachovuna ili kuepuka uwezekanao wa kukabiliwa na upungufu wa chakula.

Pia akawataka kujenga tabia ya kufanya kazi kwa bidii na kuacha uvivu.

Akasema hilo litasaidia katika kuleta maendeleo ya haraka katika jamii na Taifa kwa ujumla.

  • SOURCE: Alasiri
Habari za Leo
-----------------------------------------------
Maoni ya Mhariri
-----------------------------------------------
Business bits
-----------------------------------------------
Makala
 
Privacy Statement Terms Of Use ©1998-2007 IPPMedia Ltd.  All Rights Reserved.