|
Korogwe wapigwa tafu
2008-02-28 17:32:47
Na Azizi Issa
Serikali imetoa zaidi ya shilingi milioni 68 kwa wakazi wa vijiji tisa wilayani Korogwe.
Fedha hizo ni kwa ajili kuboresha utekelezaji miradi midogo ya kijamii na vikundi vya uzalishaji mali.
Kwa mujibu wa Ofisa Kilimo wa wilaya hiyo, Bw. Mweta Njema, pesa hizo zitatumika katika kuboresha miradi ya kilimo bora cha maharage, ufugaji kuku wa asili, mbuzi wa maziwa, matumizi ya wanyama kazi na kuhifadhi mazingira.
Akasema vijiji hivyo vilipewa pesa hizo Februari 2 mwaka huu wakati Makamu wa Rais Dk. Ali Mohamed Shein alipofanya ziara mkoani humo.
Akasema miradi hiyo ni ya uboreshaji kuku asili, hifadhi ya mazingira na ufugaji wa mbuzi wa maziwa utafanyika katika vijiji vya Kwakibomi, Gombero, Magundi na Mgila.
|