17 Jul 2006 MAIN PAGE SITE INDEX CONTACT US HELP
  Swahilinews
NAVIGATION
SEARCH
 
SPECIAL  
ARCHIVES  
Print this article Send this article

Wabunge walilia viwanja
 
2006-07-17 14:44:13
Na Mashaka Mgeta, Dodoma

Waheshimiwa wabunge wameshindwa kuzuia hisia zao na kuweka bayana kuwa, wanakosa viwanja vya ’kujirusha’ wanapokuwa mjini hapa katika siku za mwisho wa wiki.

Hayo yamesemwa na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano Mheshimiwa Samuel Sitta alipokuwa akitoa matangazo ya kawaida kwenye kikao cha Bunge la bajeti linaloendelea mjini hapa.

Mhe. Sitta akasema hatua hiyo imefikiwa na wabunge waliomfikishia ’kimemo’ wakielezea hisia zao kuhusu ukosefu wa shughuli za kustarehe maarufu kama ’kujirusha’ mjini Dodoma.

Wabunge hao ambao hata hivyo majina yao hayakuwekwa wazi wakasema, mji wa Dodoma ’umezizima’ kutokana na ukosefu wa burudani zinazoweza kuwapa fursa ya ’kujirusha’ hasa baada ya kazi nzito ya kujadili na kupitisha bajeti mbalimbali za Serikali.

Hata hivyo licha ya kutotaja majina ya wabunge waliomtumia kimemo hicho, Mhe. Sitta akasema kuna uwezekano mkubwa kwamba kilitoka kwa wabunge vijana.

Aidha, Mhe. Sitta akasema suala la kuushanikiza mji wa Dodoma kuwa na starehe zinazoweza kuwafanya wabunge kupata fursa ya ’kujirusha’ halipo chini ya mamlaka ya Bunge.

Lakini akasema hisia za wabunge hao zinaweza kuwa kichocheo kwa vijana wasanii kutoka ndani na nje ya Dodoma kutumia fursa hiyo kuja kufanya shughuli zao zinazoweza kukidhi kiu ya wabunge nyakati za mwisho wa wiki.

Kwa kawaida, wabunge wengi wanapenda kutumia siku za mwisho wa wiki kwa ajili ya kwenda Mnadani, eneo maarufu kwa upatikanaji wa nyama choma inayosindikizwa na vinywaji vya aina mbalimbali na hivyo kupata burudani ya kukidhi uchovu wa siku za katikati ya juma.

  • SOURCE: Alasiri
Habari za Leo
-----------------------------------------------
Maoni ya Mhariri
-----------------------------------------------
Business bits
-----------------------------------------------
Makala
 
Privacy Statement Terms Of Use ©1998-2005 IPPMedia Ltd.  All Rights Reserved.