


Rais Jakaya Kikwete, amemteua Bi Saada Mkuya Salum kuwa mbunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania , taarifa ya Ikulu imesema, Bi Salum aliteuliwa jana na kufanya idadi ya wabunge walioteuliwa na Rais wiki hii kufikia wanne.
Taarifa ya Kurugenzi ya Mawasilano ya Ikulu ilisema jana kuwa uteuzi huo unaanza mara moja.
Alhamisi wiki hii Rais aliwateua Profesa Sospeter Muhongo, ambaye ni mtaalamu wa jiolojia, Mwenyekiti wa NCCR Mageuzi, James Mbatia ambaye ni Mwenyekiti wa NCCR Mageuzi na Joyce Mbene kuwa wabunge wapya wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.